DKT.NCHIMBI AAGIZA KUFANYIKA UTAFITI SEKTA YA MISITU

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Emanuel Nchimbi, ameielekeza Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Taasisi ya utafiti wa Misitu Tanzania (Tafori) kufanya utafiti utakaosaidia kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili Wakulima wa Miti, hususan katika mMsitu ya asili.

Dkt. Nchimbi ametoa maelekezo hayo wakati wa ufunguzi wa Maadhimisho ya Siku ya Misitu Duniani pamoja na Kampeni ya Kitaifa ya Upandaji Miti iliyofanyika katika Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi.

RAIS SAMIA APOKEA RIPOTI YA MABORESHO YA MFUMO WA KODI

Rais Samia Suluhu Hassan amepokea Ripoti ya Tume ya Rais ya kutathmini maboresho ya mfumo wa Kodi Nchini huku akiagiza kuwepo kwa kodi ya haki na usawa kwa Wananchi pamoja na kuwa na tafsiri moja ya sheria ya kodi kati ya Mfanyabiashara na Afisa wa Kodi.

Tume hiyo iliundwa na Rais Dkt.Samia Julai 2024 ili kufanya tathimini ya kina ya Mfumo wa Kodi, kufuatia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa Wawekezaji, na Wafanyabiashara kuhusu changamoto ya mifumo ya kodi Nchini.

BANDARI YA MPIGADURI YAFANYA MAJARIBIO KUSHUSHA MIZIGO

Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum Mohamed, Amezindua Majaribio Ya Ushushaji Wa Mizigo Katika Bandari Ya Mpigaduri, Zoezi Lililofanywa Na Meli Za Kampuni Ya Azam Marine.

Akizungumza Wakati Wa Uzinduzi Huo Uliofanyika Waziri Wa Ujenzi Na Uchukuzi Ameeleza Kuridhishwa Na Majaribio Hayo, Huku Akisema Ni Sehemu Ya Jitihada Za Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Kupunguza Msongamano Katika Bandari Ya Malindi.

Amesema Kazi Rasmi La Ushushaji Mizigo Inatarajiwa Kuanza Mwezi Aprili Mwaka Huu Baada Ya Kukamilika Kwa Majaribio Ya Awali. 

DKT.MWINYI AKAMILISHA KUFUTARISHA KATIKA MIKOA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi wa Mkoa wa Kusini katika Futari ya pamoja aliyowaandalia .

MHE.AYOUB ASHIRIKI MKUTANO WA USHIRIKIANO TANZANIA NA UGANDA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, ameshiriki katika Mkutano wa Tano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission - JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda uliofanyika kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa pande mbili katika sekta mbalimbali za maendeleo.

Katika mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, wajumbe wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo mashirikiano ya kidiplomasia na kisiasa, masuala ya ulinzi na usalama pamoja na uhamiaji.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.