Wizara ya Nishati imechukuwa hatua mpya ya kuimarisha huduma za umeme Mkoani Shinyanga baada ya Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kupatiwa vitendea kazi vitakavyorahisisha kuwafikia wananchi wengi zaidi, hususan waishio vijijini na maeneo ya pembezoni.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Stephen Wasira, amewatahadharisha wanachama wa chama hicho kuacha tabia ya kuanzisha mivutano na uchochezi wanapokosa fursa za uteuzi au kushindwa katika kura za maoni.
Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) imeendesha mafunzo maalum kwa Maafisa Ugani kata 75 wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha sekta ya kilimo kama mhimili mkuu wa uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.