Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Imejipanga Kuhakikisha Inaweka Mazingira Mazuri Na Wezeshi Kwa Wazee Kwa Kuwajengea Makaazi Mazuri Na Salama Ya Kuishi Ili Kuondokana Na Changamoto Za Makaazi.
Hayo Yameelezwa Na Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Katika Ziara Yake Mkoa Wa Mjini Magharibi Baada Ya Kukagua Mradi Wa Ujenzi Wa Nyumba Za Wazee Welezo.
Amesema Serikali Itaendelea Kuwathamini Na Kuwatunza Wazee Kwa Kuhakikisha Wanapatiwa Mahitaji Yote Muhimu Ikiwemo Kuishi Katika Mazingira Mazuri, Rafiki Na Wezeshi Kulingana Na Uhitaji Wao.