RAIS SAMIA ATAKA MAMA NA BABA LISHE WAHESHIMIWE

Rais Wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Amemtaka Waziri Wa Tamisemi Prof. Riziki Shemdoe Kutenga Na Kuyaendeleza Maeneo Yaliyo Kwisha Tengwa Kwa Ajili Ya Shughuli Za Mama Na Baba Lishe Nchini Pamoja Na Kuweka Miundombinu Bora Huku Mama Na Baba Lishe Wakitakiwa Kutumia Nishati Safi Ya Kupiki Katika Shughuli Zao.

Pia Rais Dkt Samia Ameitaka Wizara Ya Fedha Kuweka Mazingira Rafiki Ya Kisera Na Kisheria Ili Wafanyabiashara Ndogondogo Wakiwemo Mama Na Baba Lishe Nchini Waweze Kunufaika Na Mikopo Inayotolewa Na Serikali.

SERIKALI YAIMARISHA MAKAAZI YA WAZEE

Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Imejipanga Kuhakikisha Inaweka Mazingira Mazuri Na Wezeshi Kwa Wazee Kwa Kuwajengea Makaazi Mazuri Na Salama Ya Kuishi Ili Kuondokana Na Changamoto Za Makaazi.

Hayo Yameelezwa Na Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Katika Ziara Yake Mkoa Wa Mjini Magharibi Baada Ya Kukagua Mradi Wa Ujenzi Wa Nyumba Za Wazee Welezo.

Amesema Serikali Itaendelea Kuwathamini Na Kuwatunza Wazee Kwa Kuhakikisha Wanapatiwa Mahitaji Yote Muhimu Ikiwemo Kuishi Katika Mazingira Mazuri, Rafiki Na Wezeshi Kulingana Na Uhitaji Wao.

ZANZIBAR YAKABILIWA NA UHABA WA WATAALAMU WA USONJI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema hali ya Usonji kwa Watoto ni changamoto kubwa katika Jamii, hivyo Serikali ina wajibu wa kuhakikisha inaunga mkono jitihada za kuwasaidia Watoto wanaoathirika na hali hiyo.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.