Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.
Hayo yamezungumzwa na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Juma Homera mara baada ya kuwasha umeme rasmi katika kitongoji cha Ujamaa na Kisutu vilivyopo wilaya ya Namtumbo mkoani humo.