TANESCO YAJIPANGA KUHUDUMIA VITONGOJI 400, HANANG

Shirika la umeme Tanzania (Tanesco) Wilayani Hanang Mkoani Mnayara limejipanga  kuboresha huduma za matengenezo na maboresho ya huduma za umeme katika vitongoji zaidi ya 400 baada ya kupatiwa gari la mtambo linalotoa huduma mbali mbali ikiwemo kubadilisha nguzo na mashine umba maarufu kama transfoma.


 

SERIKALI SMT YAAGIZA KUPEWA MATIBABU BURE KIJANA MARTIN JOSEPH

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga  kwa niaba ya Mhe.Waziri Mkuu dkt.Mwigulu Nchemba  amekabidhi kiti mwendo  kwa kijana mwenye ulemavu Martin Joseph mkazi wa Babati,baada ya familia ya kijana huyo kuomba msaada kwa waziri mkuu alipokuwa kwenye ziara yake mwezi  machi /2026 mkoani humo.

REA YAWASHA UMEME VITONGOJI 307 NAMTUMBO

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imewekeza jumla ya shilingi bilioni 12.1 katika miradi ya kupeleka umeme kwenye vitongoji katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.

Hayo yamezungumzwa na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Juma Homera mara baada ya kuwasha umeme rasmi katika kitongoji cha Ujamaa na Kisutu vilivyopo wilaya ya Namtumbo mkoani humo.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.