MIUNDO MBINU BORA YA BARABARA NI CHACHU YA MAENDELEO

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Zanzibar Dkt.Khalid Salum Mohamed amesema lengo la Serikali la kuendelea kujenga miundombinu ya Barabara ni kurahisisha shughuli za usafiri na usafirishaji kwa Wananchi na Taifa.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Dkt .Khalid Salum Mohamed akizungumza wakati wa Ziara ya kukagua vifaa vya ujenzi wa Barabara vya Kampuni ya CCECC amesema vifaa hivyo vimekuja wakati sahihi na vitarahisisha ujenzi wa Barabara za Mjini 

 

KITUO CHA UMEME IFAKARA CHACHOCHEA MAENDELEO KILOMBERO

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imetumia shilingi bilioni 25 kujenga Kituo cha Kupoza Umeme 1x20MVA, 220/33kv pamoja na njia za kusambaza Umeme katika Wilaya ya Kilombero, hatua ambayo imeboresha upatikanaji wa umeme na kuondoa changamoto ya kukatika kwa nishati hiyo katika wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi.

KAMATI YA BARAZA LA WAWAKILISHI YARIDHISHWA NA MIRADI YA UBORA UWANJA WA AAKIA

Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Miundombinu, Ardhi na TEHAMA imeeleza kuridhishwa na maendeleo ya miradi ya ujenzi na maboresho ya miundombinu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA), ikisema miradi hiyo inakidhi viwango vya kimataifa na itachangia kwa kiasi kikubwa kukuza sekta ya usafiri wa anga na uchumi wa Zanzibar.

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.