VIONGOZI WAHAMASISHWA KUWASAIDIA WANANCHI

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Amewahamasisha Viongozi Kuwasaidia Wananchi Hasa Katika Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani Ili Kuweza Kuweka Uwiano Sawa Wa Mahitaji.

Mhe. Hemed Ambae Ni Mwakilishi Wa Jimbo La Kiwani, Ametoa Wito Huo Baada Ya Ugawaji Wa Futari Kwa Wananchi Wa Jimbo Hilo Shehia Ya Kendwa Yenye Nyumba Zaidi Ya 1156 Hafla Iliyofanyika Kwenye Uwanja Wa Mpira Wa Mauwanifutari Kwa Wananchi Wote Hasa Wenye Mahitaji Maalum.

WANAOSAFIRISHA MAGENDO WATAKIWA KUCHUKULIWA HATUA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya ameagiza kuchukuliwa hatua kali za kisheria dhidi ya wale waliohusika kutaka kutorosha Magunia 15 ya Karafuu katika Bandari ya Wambaa Wilaya ya Mkoani

MFUMO MPYA WA KUSAMBAZA DAWA ZA KULEVYA WAGUNDULIWA

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar imewakamata Watuhumiwa Watatu wanaosadikiwa kusambaza na kuuza Dawa za kulevywa kwa kutumia mbinu mpya ambayo ni kuchanganya na Dawa za Binaadamu

Akitoa Taarifa kwa Waandishi wa Habari Ofisini kwake Migombani Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar Kanali Burhani Zubeiri Nassoro amesema bidhaa hizo zenye vifungashio zimekamatwa katika Maduka mabali mbali hapa Zanzibar

Subscribe to
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.