KARUME BOYS U-15 YAKABIDHIWA MILIONI MIA MOJA NA SITA, LAKI SABA NA TISINI.
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar imekabidhi kiasi cha fedha kwa timu ya taifa ya Zanzibar kufuatia harambee iliyofanywa katika fainali waliyoifunga Uganda na kutwaa Ubingwa wa CECAFA chini ya umri wa miaka 15 hivi karibuni.
Katika harambee hiyo kiasi kilichopatikana ni Shilingi Milioni Mia Moja na sita, laki Saba na Tisini huku kila mchezaji amekabidhiwa Shilingi Milioni Mbili na Laki Tisa kwa wachezaji 25 na Viongozi 10, ambapo Jumla ni 35 wanaounda Timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 15.