KATIBU NEC ATEMBELEA MIRADI YA AFYA HOSPITALI YA RUFAA KILIMANJARO

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa (SUKI), Rabia Abdalah, ambaye pia ni mlezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Kilimanjaro, ametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kilimanjaro kwa lengo la kujionea utekelezaji wa baadhi ya miradi ya maendeleo inayoendelea katika hospitali hiyo.

ACT WAZALENDO YAIOMBA ZEC KUSIMAMISHA UCHOMAJI NYARAKA ZA UCHAGUZI

Chama cha ACT Wazalendo Zanzibar kimeiomba Tume ya Uchaguzi Zanzibar–ZEC kusimamisha zoezi la uteketezaji wa nyaraka na vifaa vya Uchaguzi kwa kile walichodai ni mpaka mashauri yaliyoko Mahakamani yamalizike.

Kauli hii imekuja kutokana na Tamko la Tume ya Uchaguzi lililotolewa hapo Jana likieleza nia ya Tume kuteketeza nyaraka zote za Uchaguzi wa Mwaka 2025 kwa baada ya Siku 90 kwa mujibu wa Sheria.

UWEKEZAJI ZANA ZA KILIMO AFRIKA HAIENDANI NA MAHITAJI HALISI

Tanzania Kwa Kushirikiana Na Shirika La Kilimo Na Chakula La Umoja Wa Mataifa (Fao) Imeandaa Mkakati Wa Taifa Wa Zana Za Kilimo Unaolenga Kuimarisha Matumizi Ya Uzalishaji, Usimamizi Na Uratibu Wa Teknolojia Za Kilimo.

MHE. HEMED ATIA SHIME UPATIKANAJI WA DAWA ZA KISUKARI

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Amesema Serikali Inawajibu Wa Kuweka Mazingira Wezeshi Kupitia Sera Madhubuti, Ufadhili Endelevu Na Ushirikiano Utakao Hakikisha  Changamoto Kubwa Ya Ukosekanaji Wa Dawa Ya Insulini Kwa Watu Wanaoishi Na Ugonjwa Wa Kisukari Inapatiwa Ufumbuzi Wa Haraka.

MADIWANI MBULU WATAKA WASIOCHANGIA CHAKULA SHULENI WACHUKULIWE HATUA

Baraza la madiwani wa halmashauri ya mji wa Mbulu mkoani Manyara wameiomba Serikali  kuwachukulia hatua kali za kisheria Wazazi wasiochangia chakula kwa watoto wao shuleni ili kuwezesha watoto kupata chakula cha mchana na kuinua kiwango cha taaluma.


Madiwani hao Wametoa Ombi hilo wakati wa kikao cha kwanza cha baraza hilo ambapo wamelalamikia tabia ya baadhi ya wazazi kutochangia mchango wa chakula shuleni kwa watoto wao hali inayokuwa kikwazo kwa jitihada za kuinua taaluma na kuondokana na utoro shuleni.

MAHAKAMA YAPENI KIPAUMBELE MASHTAKA YA UKATILI DC KAGANDA.

Serikali Mkoani Manyara imeishauri mahakama kuyapa kipaombele mashauri yanayohusu ukatili wa kijinsia na kutoa adhabu yenye kuleta majuto kwa jamii na wanaohusika na matukio hayo.


Kauli hiyo kwa mahakama Kanda ya Manyara imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Babati Emanuela Kaganda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga wakati akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya sheria Nchini yaliyofanyika kwenye viwanja vya mahakama hiyo Mkoani humo.

ZANZIBAR YASAINI MRADI WA KUIMARISHA MIUNDOMBINU

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesaini Mkataba wa Miaka Mitano na Czech–Tanzania Development Chamber of Commerce, unaolenga kuimarisha miundombinu na kuchochea uchumi endelevu wa Zanzibar. 

Miongoni mwa Maeneo yatakayotekelezwa ni Sekta ya usafiri wa Anga na Barabara ya Reli na Miradi mingine ya kimkakati ili kuongeza fursa za kiuchumi. 

MAFUNZO YA UTUMISHI KWA WAFANYAKAZI NI MUHIMU KAZINI

Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni inayotoa huduma za bima zinazozingatia misingi na sharia ZIC Takaful Ndg.Said Abdallah Basleym amesema suala la Mafunzo kwa Wafanyakazi ni jambo la kupewa kipaumbele ili kuhakikisha wanaendana na kasi ya utendaji na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.

Akizungumza wakati wa Mafunzo ya kujenga uwezo yaliyotolewa kwa Wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Ndg. Said ameeleza kuwa uwekezaji katika Mafunzo husaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa Kampuni, pamoja na kuboresha huduma zinazotolewa kwa Wananchi.

MHE. HEMED APONGEZA MCHANGO WA TAASISI ZA DINI KUSIMAMIA MAADILI

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah Amesema Serikali Inatambua Na Kuthamini Mchango Wa Viongozi Wa Dini Katika Kuimarisha Amani, Maendeleo Na Maadili Mema Kupitia Mafundishoya Dini.

Mh. Hemed Suleiman Ametoa Kauli Hiyo Wakati Akizungumza Katika Uzinduzi Wa Mashindano Ya Qur’an Ya Mabara Yote Ulimwenguni Yanayo Ratibiwa Na Taasisi Ya Al Hikma Jijini Dar Es Salaam

Huku Akiwasihi Wanamchi Kuendelea Kushikamana Katika Kulinda Na Kutunza Amani Ya Nchi.

TANESCO LINDI YAWANASA WATU WAWILI KWA KUJIUNGANISHIA UMEME KINYUME CHA SHERIA

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeendesha oparesheni maalumu ya kudhibiti vitendo vya kujiunganishia umeme kiholela na kinyume cha sheria, ambapo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wanaodaiwa kujiunganishia huduma hiyo bila kufuata taratibu.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.