SMZ IMEFANYA MAPINDUZI MAKUBWA KWENYE SEKTA YA AFYA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Mngereza Mzee Miraji, ameeleza kwa kina dira ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ya kuiondoa Zanzibar katika utegemezi wa rufaa za matibabu nje ya nchi na badala yake kuijenga kuwa kitovu muhimu cha huduma za afya katika ukanda wa Afrika Mashariki.

ZANZIBAR INAENDELEA KUPIGA HATUA KWENYE SEKTA YA UTALII KIMATAIFA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe Akizungumza katika tathmini ya utekelezaji wa siku 100, amesema Zanzibar imeendelea kufanya vizuri na kujipatia nafasi kwenye orodha mbalimbali za kimataifa za utalii.

Ameeleza kuwa Zanzibar sasa ipo katika kumi bora barani Afrika kwenye vivutio vya utalii, miradi bora ya kitalii, maeneo bora ya honeymoon pamoja na michezo ya baharini, hali inayoongeza ushindani na kuimarisha nafasi ya Zanzibar katika soko la kimataifa la utalii.

ZANZIBAR SEKTA YA UTALII INAKUA KWA KASI, ZAIDI YA WATALII LAKI 1 WANATEMBELEA KWA MWEZI

Baada ya kuapishwa kwa Mhe. Rais  Dkt. Hussein Mwinyi kuongoza Zanzibar katika awamu ya nane ya uongozi, sekta ya utalii imeonesha ukuaji mkubwa na wa kasi. Katika mwezi wa kwanza wa uongozi huo, idadi ya watalii ilikuwa takribani elfu 72 pekee.
Hata hivyo, kwa sasa kuanzia Novemba hadi Januari, Zanzibar inapokea wastani wa watalii laki 1 kwa kila mwezi.

DKT. SAMIA AWAHIMIZA WATENDAJI KUWAJIBIKA

Raisi Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan Amewaapisha Viongozi Aliowateua Hivi Karibuni Na Kuwataka Kuwajibika Ipasavyo Ili Kufanikisha Utekelezaji Wa Dira Ya Taifa.

Hafla Hiyo Ya Uapisho Iliyofanyika Ikulu Ya Magogoni Jijini Dar Es Salaam, Iliwahusisha Wakuu Wa Mikoa, Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala Wa Mikoa, Naibu Makatibu Wakuu, Katibu Mtendaji Wa Tume Ya Mipango, Naibu Katibu Mtendaji Wa Tume Ya Mipango, Na Balozi Iliambatana Na Kiapo Cha Ahadi Ya Uadilifu Wa Watumishi Wa Umma.

TAASSI ZA ELIMU ZASISITIZWA KUWEKEZA KWENYE UTAFITI

Wito Umetolewa Kwa Taasisi Binafsi Kushirikiana Vyema Na Taasisi Za Elimu Pamoja Na Kuekeza Katika Tafiti Hususan Za Kisayansi Na Teknolojia Kuhimiza Ubunifu Katika Ufundishaji Na Ujifunzaji Ili Kuinua Viwango Vya Tafiti Na Ubora Wa Elimu.

Wito Huo Umetolewa Jijini Dar Es Salaam Na Makamu Wa Rais Wa

SMZ YAWEKEZA ZAIDI YA SH. BIL. 13 KATIKA MAHAKAMA

Serikali Ya Mapinduzi Ya Zanzibar Imechukua Hatua Thabiti Ya Kuweka Mazingira Bora Ya Kufanyia Kazi Kwa Mhimili Wa Mahakama.

Amesema Katika Mwaka Wa Fedha 2025/2026 Serikali Imewekeza Zaidi Ya Fedha Za Kitanzania Shilingi Bilioni 13.6 Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Majengo Ya Kisasa Ya Mahakama Ambayo Yanaendana Na Uwekaji Wa Miundombinu Ya Tehama.

Baada Ya Shamrashamra Ya Wiki Ya Sheria, Hatimae Kilele Cha Maadhimisho Hayo Yamefanyika Kisiwani Pemba.

WAZIRI MKUU ACHUKIZWA NA MIGOGORO YA ARDHI

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewasisitiza Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya pamoja na watumishi wa umma wahakikishe wanatenga muda wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika maeneo yao hususani kwenye migogoro ya ardhi katika ngazi zao za kiutawala. 
 
Ameyasema hayo leo Ijumaa, Februari 6, 2026 wakati wa kuahirisha Mkutano wa Pili wa Bunge la 13 jijini Dodoma, akisisitiza kuwa viongozi hao wanapaswa kuwafuata wananchi, kuwasikiliza na kuchukua hatua za haraka za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wakiwa katika maeneo yao.

DKT. MWINYI KUFUNGUA IJTIMAI ZANZIBAR

Rais Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Kesho Anatarajiwa Kuwa Mgeni Rasmi Katika Ufunguzi Wa Ijtimai Ya Kimataifa Itakayofanyika Katika Eneo La Fuoni Migombani.

Maandalizi Ya Ijitimai Hiyo Tayari Yamekamili Huku Waumini Wa Dini Ya Kiislamu Wakihimizwa Kuhudhuria Katika Ijitimai Hiyo Ambayo Itawakumbusha Mambo Ya Heri Na Kumcha Mwenyezi Mungu.

WADAU WA USALAMA BARABARANI WATAKIWA KUSHIRIKIANA

Mkuu Wa Mkoa Wa Mjini Magharibi, Moh’d Abdalla Ali, Amesema Wafanyabiashara Wa Soko La Mombasa Wanatarajiwa Kuanza Kufanya Biashara Zao Ndani Ya Soko Hilo Katika Kipindi Cha Hivi Karibuni.

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari, Mheshimiwa Mohd Abdalla Ali Amesema Tayari Wameshagawa Vizimba Kwa  Wafanya Biashara Na Wanatarajia Kuanza Kulitumia Soko  Kabla Ya Mwezi Wa Ramadhani

ZBC YATUNUKU ZAWADI KWA WAFANYAKAZI BORA

Mwenyekiti Wa Bodi Ya Shirika La Utangazaji Zanzibar Zbc Mhandisi Idrisa Muslim Hijja Amesema Ili Kufikia Dhamira Ya Serikali Kuimarisha  Maendeleo Ni Muhimu Kwa Wafanyakazi Kujituma Zaidi Katika Kutekeleza Majukumu Yao

 

Akizungumza Katika Hafla Ya Kuwapongeza Wafanyakazi Wa Shirika Za Utangazaji Zbc Waliofanya Vizuri Kwa Mwaka Huu Kupitia Hafla Maalum Ya Utoaji Tuzo Amesema Hatua Inalenga Kuimarisha Uwajibikaji ,Ubunifu Na Kuongeza Motisha Katika Kufanya Kazi

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.