WANAWAKE 6,500 HUFARIKI KILA MWAKA KUTOKANA NA SARATANI YA MLANGO WA KIZAZI

Taarifa ya wiki ya chanjo

     WANAWAKE Zaidi ya 9,500 kati ya 100,000 hugundulika kila mwaka kuwa na tatizo la saratani ya mlango wa kizazi,kati yao wanawake 6,500 hufariki dunia kila mwaka.

      Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dr.Louis Chomboko wakati anatoa taarifa ya maadhimisho ya wiki ya chanjo na uzinduzi wa dozi moja ya chanjo dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi (HPV) kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.

     Dr.Chomboko amesema inakadiriwa wanawake Zaidi ya 450,000 wamethibitika kuwa na saratani ya mlango wa kizazi duniani na wengi wao wapo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania.

    “Saratani ya mlango wa kizazi inashika nafasi ya pili kwa kusababisha saratani kwa wanawake ulimwenguni,nafasi ya kwanza inashikwa na saratani ya matiti’’,alisisitiza.

     Hata hivyo Dr.Chomboko amesema hapa nchini saratani ya mlango wa kizazi inaongoza miongoni mwa saratani zote zinazogundulika miongoni mwa wanawake wenye umri wa kuanzia miaka 15 hadi 44.

    Ameyataja mambo yanayochochea kupata saratani ya mlango wa kizazi kuwa ni kuanza kujamiana katika umri mdogo,kuwa na wapenzi wengi,kuwa na ndoa za mitaala,uvutaji sigara,kuwa na mpenzi asiyetahiriwa na virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

      Amezitaja dalili za saratani ya mlango wa kizazi kuwa ni kutokwa damu bila mpangilio,maumivu ya mgongo,kuchoka,kutoka uchafu kwenye uke, kuishiwa damu,figo kushindwa kufanya kazi, uvumbe wa tezi na kupatwa na fistula.

 

Tags
stories
standard
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.