VIONGOZI WAHAMASISHWA KUWASAIDIA WANANCHI

Makamu Wa Pili Wa Rais Wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla Amewahamasisha Viongozi Kuwasaidia Wananchi Hasa Katika Kipindi Cha Mwezi Mtukufu Wa Ramadhani Ili Kuweza Kuweka Uwiano Sawa Wa Mahitaji.

Mhe. Hemed Ambae Ni Mwakilishi Wa Jimbo La Kiwani, Ametoa Wito Huo Baada Ya Ugawaji Wa Futari Kwa Wananchi Wa Jimbo Hilo Shehia Ya Kendwa Yenye Nyumba Zaidi Ya 1156 Hafla Iliyofanyika Kwenye Uwanja Wa Mpira Wa Mauwanifutari Kwa Wananchi Wote Hasa Wenye Mahitaji Maalum.

WANAOSAFIRISHA MAGENDO WATAKIWA KUCHUKULIWA HATUA

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mgeni Khatib Yahya ameagiza kuchukuliwa hatua kali za kisheria dhidi ya wale waliohusika kutaka kutorosha Magunia 15 ya Karafuu katika Bandari ya Wambaa Wilaya ya Mkoani

MFUMO MPYA WA KUSAMBAZA DAWA ZA KULEVYA WAGUNDULIWA

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar imewakamata Watuhumiwa Watatu wanaosadikiwa kusambaza na kuuza Dawa za kulevywa kwa kutumia mbinu mpya ambayo ni kuchanganya na Dawa za Binaadamu

Akitoa Taarifa kwa Waandishi wa Habari Ofisini kwake Migombani Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Zanzibar Kanali Burhani Zubeiri Nassoro amesema bidhaa hizo zenye vifungashio zimekamatwa katika Maduka mabali mbali hapa Zanzibar

WATOTO WENYE ULEMAVU WATOA KILIO CHAO HADHARANI

Wadau wa Maendeleo, Watunga Sera, Mashirika yasiyo ya Kiserikali pamoja na asasi za kiraia kutoka Nchi 23 Duniani wamekutana Jijini Arusha katika Jukwaa la Kimataifa la kujifunza kuhusu usawa wa kijinsia, ujumuishi wa watu wenye ulemavu na ushirikishwaji wao katika Jamii.

SERIKALI KUMALIZA MIGOGORO YA ARDHI IFIKAPO 2030

Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Mhe. Rahma Kassim Ali ameeleza azma ya Serikali ni kumaliza migogoro ya ardhi ifikapo 2030 kupitia Mradi wa Mfumo wa Usimamizi na Usajili wa Ardhi (laris).

DKT. MWIGULU AAGIZA KUCHUKULIWA HATUA MKANDARASI MANYARA

Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, kumchukulia hatua Mkandarasi wa mradi wa kuboresha miundombinu ya Miji Tanzania (Tactics).

Agizo hilo amelitoa kufuatia kucheleweshwa kwa mradi huo wenye thamani ya Shilingi Bilioni 19.9, unaojumuisha Ujenzi wa Bararaba, Mitaro pamoja na Ujenzi wa Stendi ya Mkoa wa Manyara ambapo mpaka sasa Ujenzi wa stendi hiyo umefikia asilimia 10 tu.

SERIKALI KUTUMIA BILIONI 79 KUJENGA VITUO VYA POLISI 698 NCHI NZIMA

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, amesema Serikali imepanga kutumia zaidi ya Shilingi Bilioni 79 kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi 698 nchini, ikiwa ni mkakati wa kuimarisha usalama wa raia na mali zao.

​Akizungumza leo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya Vituo vya Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar Mhe. Ayoub Mahmoud amebainisha kuwa uamuzi huo umekuja baada ya Serikali kuona kuna uhitaji wa kusogeza huduma za Kipolisi karibu na wananchi zaidi.

KIKOSI CHA ZIMAMOTO CHAPOKEA GARI TISA NA BOTI 1

Kamishna wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar Rashid Mzee Abdallah amesema Kikosi hicho kinaendelea kujiimarisha kwa kuwa na Vifaa vya kisasa vya kukabiliana na Majanga ya Moto.

 

Kamishna Rashid ameyasema hayo baada ya kupokea Gari Tisa za Kuzimia Moto na Boti moja kutoka Nchini Austria.

BILIONI MIA SABA ZATUMIKA KUJENGA KIWANDA CHA SUKARI KILOMBERO

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mipango na uwekezaji Professa Kitila Mkumbo amesema kiwanda kipya cha sukari Kilombero K4  kilichopo Mkoani Morogoro ambacho kinajengwa kwa gharama ya shilingi Billioni mia saba kinatarajiwa kuanza uzalishaji wake Mwezi Juni Mwaka huu ni moja ya Kiwanda ambacho kitafanya lengo ya kukuza uchumi kuelekea Mwaka 2050  kufikia dola trilioni moja.

DKT. MKUYA ATAKA WACHUKULIWE HATUA WAHUDUMU WASIOWASIJIBIKA

Kaimu Waziri Wa Afya Zanzibar Na Waziri Wa Nchi Afisi Ya Raisi Ikulu Dkt Saada Mkuya Salum Amewataka Madaktari Dhamana Ngazi Ya Wilaya Kufanya Kazi Kwa Weledi Ili Sekta Ya Afya Ieandane Na Uwekezaji Uliofanywa Na Serikali.

Akizungumza Katika Mkutano Maalumu Na Viongozi Wa Wizara Ya Afya Pamoja Na Madaktari Hao Dkt. Saada Amesema Kwa Sasa Wananchi Wamekuwa Wakilalamikia Juu Ya Huduma Wanazozipata Katika Vituo Vya Afya Pamoja Na Hospitali, Jambo Ambalo Limekuwa Likiongeza Matatizo Kwa Wagonjwa Wanaofuata Huduma Katika Hospitali Hizo.

Subscribe to news
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.