IGP WAMBURA ATANGAZA MABORESHO MAKUBWA VITUO VYA AFYA VYA POLISI
Mkuu wa Jeshi la Polisi amesema vituo tiba vitaendelea kuboreshwa katika eneo la miundombinu, vifaa tiba na kuwekeza katika raslimali watu ikiwemo kuajiri wataalamu wapya wa Afya.
IGP Wambura ameyasema hayo mkoani Morogoro wakati akifungua mkutano wa Wakuu wa vituo tiba, Wahasibu na Watendaji wa Kikosi cha Afya.
Alisema Jeshi la Polisi linaendelea kuboresha matumizi ya TEHAMA hivyo amewataka kuwa wepesi katika kujifunza na kutumia mifumo iliyopo ili kutoa huduma bora kwa wateja wa ndani na nje wanaopata huduma katika hospitali za Polisi.
