BILIONI MIA SABA ZATUMIKA KUJENGA KIWANDA CHA SUKARI KILOMBERO
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mipango na uwekezaji Professa Kitila Mkumbo amesema kiwanda kipya cha sukari Kilombero K4 kilichopo Mkoani Morogoro ambacho kinajengwa kwa gharama ya shilingi Billioni mia saba kinatarajiwa kuanza uzalishaji wake Mwezi Juni Mwaka huu ni moja ya Kiwanda ambacho kitafanya lengo ya kukuza uchumi kuelekea Mwaka 2050 kufikia dola trilioni moja.
