Michezo

MPIRA WA MIGUU UNAENDESHWA KWA SHERIA NA KANUNI NA SIO MIHEMKO

     Rais wa shirikisho la mpira wa Miguu Zanzibar, Suleiman Mahmoud Jabir amesema kuwa “Mpira wa miguu unaendeshwa kwa sheria na kanuni zake sio kwa mihemko ya baadhi ya watu”

    Rais wa ZFF ameyasema hayo wakati akifungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Magharibi B katika Skuli ya Samia Suluhu Hassan iliyopo Mwanakwerekwe.

     Amesema Mkutano Mkuu ndiyo chombo muhimu katika kupanga mambo mbali mbali ya Wilaya husika pamoja na mipango ya uendeshaji wa Mpira kwa wilaya husika.

VIJANA 49 WAPATIKANA KWENYE KUSAKA VIPAJI

Katibu Mkuu Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) Hussein Ahmada amesema jumla ya Vijana 49 wamepata fursa ya

kuchaguliwa kwenye zoezi maalum la kusaka Vipaji vya Vijana

Wadogo.

Hussein Ahmada amesema chini ya Umri wa Miaka 15 wamepatikana Vijana 22 na chini ya umri wa Miaka 17 wamepatikana Vijana 27 katika zoezi hilo.

Hussein amewaomba Wazazi kuwaunga Mkono Vijana wao katika kufanikisha mafanikio ya Mpira wa Miguu Zanzibar.

Zoezi hilo la kusaka Vipaji vya Wachezaji Vijana imeandaliwa

SIMBA NA YANGA KIBARUA KIZITO LEO

   Meneja Habari na Mawasilino wa Klabu ya Simba Ahmed Ali amesema Kikosi chao kiko vyema kuwakabili Al-ahly ya Misri licha ya kupoteza Mchezo wao wa Awali.

    Ahmed amesema wamefanya Mazoezi yao ya Mwisho kuelekea Mchezo huo na hawana wasi wasi juu ya kupindua meza na kutinga Nusu Fainali.

    Aidha Ahmed amesema haitakuwa rahisi kupata Matokeo lakini wamejipanga vyema na wako tayari kupambana.

TFF YAANZA MIKAKATI YA KUIBUA VIPAJI

   Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeanza mkakati wa kuibua Vipaji vya Mpira wa Miguu kwa kuzipatia Mipira Mia Mbili Arobaini Shule za Msingi Sita za Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro 

    Akikabidhi Mipira hiyo kwa Walimu wa Shule hizo za Msingi Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) Paschal Kihanga amesema lengo la TFF na Serikali ni kuhakikisha wanatengeneza Vipaji vya Mpira kuanzia Watoto Wadogo.

SERIKALI KUGHARAMIA MASHABIKI YANGA KWENDA KWA MADIBA

    Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeunga Mkono Sekta ya Michezo kwa kugharamia Safari ya kuwasafirisha Mashabiki wa Timu ya Yanga kwa ajili ya Kwenda Nchini South Afrika katika Mechi ya Marudiano na Mamelod  Sundown.

     Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Khamis Mohamed Mwinjuma kwenye ghafla ya kuwaaga Mashabiki na Viongozi wa Timu hiyo kuelekea Nchini South Afrika iliyofanyika Makao Makuu ya Klabu hiyo Jijini Dar es salaam.

MASHINDANO YA BEACH SOKA KUFANYIKA APRIL 27

Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar kupitia Kamati ya Soka la Ufukweni imeandaa Mashindano ya Kimataifa ya Mpira wa Ufukweni kwa lengo la kuvitangaza vivutio vya Utalii vilivyopo Nchini.

Akitoa taarifa mbele ya Vyombo vya Habari, katibu Kamati ya Soka la ufukweni Zanzibar, Ali Sharifu Adolf, huko Mbuyu Mnene.

Amesema Mashindano hayo yatashirikisha timu 4 kutoka Unguja na yatafanyika katika Fungu la Mchanga la Nakupenda Sand Bank.

Adolf amewaomba Wahisani na Wadhamini mbali mbali kuwaunga mkono ili kufikia lengo la Mashindano hayo.

MACHICHA YAIGARAGIZA B5 MASHINDANO YA SWALA AIR CARCO

     Timu ya Mpira wa Miguu ya Machicha FC  imefanikiwa kuondoka na ushindi wa Penalty 5-4 dhidi ya Timu ya B5, katika Michuano ya Swala Air Cargo Ndg.Ramadhan CUP, yanayoendelea Viwanja vya Mau.

    Mchezo huo uliokuwa mgumu kwa Timu zote Mbili Mbili, licha ya Mashambulizi ya mara kwa mara, lakini kila mmoja alilinda vyema lango lango lake lisitikiswe wavu, na kupelekea Dakika 90 kukamilika kwa Sare Tasa ya bila ya kufungana.

WAZIRI TABIA ATANGAZA KUREJESHA KAMATI YA SAZI

     Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo imetangaza kurejesha tena Kamati ya Saidia Zanzibar Ishinde (SAZI) ili kuisaidia Serikali kutafuta Fedha za kuziendesha Timu za Taifa Zanzibar.

      Akitoa Taarifa kwa Vyombo vya Habari huko Ofisini kwake Migombani Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo Mhe.Tabia Maulid Mwita amesema hatua hiyo ni muhimu katika kujenga mazingira ya Ushindi na Hamasa kwa Michezo hapa Zanzibar.

MICHEZO KUTUMIKA KUREKEBISHA TABIA

    Kampuni ya Sarnity Tour wamekabidhi Vifaa vya Michezo kwa Waraibu wa Kitengo cha Tiba, Kinga na Kurekebusha Tabia Kidimni ili kutoa fursa ya Michezo Kituoni hapo.

    Wakikabidhi Vifaa vya Michezo katika Kituo cha kinga Tiba na kurekebisha tabia Meneja wa Kampuni ya Sarnity Ndg. Florence Agustino amesema lengo la kutoa Vifaa hivyo ni kutoa Fursa kwa Waraibu wa Kituo hicho ili kushiriki Michezo wakat wakiendelea na kupatiwa Elimu juu ya kuchana na utumiaji wa Madawa ya kulevya.

PBZ YAAHIDI KUIUNGA MKONO FARAFA SPORTS AWARDS

Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ ) imeahidi kushirikiana na Taasisi ya Farafa Sports Awards kufanikisha Tuzo za wana Michezo Zanzibar zinazotarajiwa kutolewa Mwezi Mei, 2024.

Meneja Masoko na kuendeleza Biashara kutoka Pbz, Seif Suleiman Mohamed huko Mpirani, amesema Benki imeamua kuwaunga Mkono Taasisi ya Farafa ili kufanikisha tukio la utoaji Tuzo za Wanamichezo hapa Zanzibar.

Katibu Mkuu Taasisi ya Farafa Sports Awards, Ali Rashid Pizaro amesema wanaishukuru PBZ na kusema kuwa lengo la tuzo hizo ni kurejesha Hamasa na Mvuto katika Michezo mbali mbali.

Subscribe to Michezo
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.