NDANI YA SIKU 100 WIZARA TUMEFANIKIWA KUTOA AJIRA 2,300
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Zanzibar, Dkt. Mngereza Mzee Miraji, ameeleza utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Afya kuanzia ngazi ya msingi hadi ngazi ya juu ya rufaa, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mfumo wa huduma za afya Zanzibar.
Ndani ya siku 100 za utekelezaji, Wizara imefanikiwa kuajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii 2,300, hatua iliyopanua upatikanaji wa huduma za afya mashinani, sambamba na kuhakikisha mishahara inalipwa kwa wakati kutokana na uongozi na maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi.


