JELA MAISHA AKITUHUMIWA KULAWITI MWANAFUNZI WA MIAKA MITANO
Mkazi mmoja wa kata ya Mkata wilaya ya Handeni Mkoani Tanga Said Mbezi (23) amehukumiwa kifo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka mitano.
Hukumu hiyo imetolewa Jumatano Januari 21,2026 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Pangani Fransisca Magwiza baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.
Awali ilielezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo mnamo Oktoba 15,2024 katika kijiji cha Mkwaja wilaya ya Pangani kwa kumlawiti kijana wa miaka mitano ambae ni mwanafunzi wa darasa la awali.
