TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA NCHI ZA NODIKI KATIKA SEKTA YA AFYA
Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden umeratibu ushiriki wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uzinduzi wa Mkutano wa Afya kati ya nchi za Nodiki na Afrika uliofanyika tarehe 22 Januari, 2026, jijini Stockholm, Sweden, ili kujadiliana masuala ya afya ya uzazi na mtoto na mapambano dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza.










