SEKTA YA AFYA ZANZIBAR NI YA KUPIGIWA MFANO
Lusi Nikolaieva Raia wa Ukraine ameisifu Sekta ya Afya Zanzibar kwa kuwekeza katika huduma ya Mama na Mtoto iliyomsaidia kujifungua salama hapa Zanzibar tofauti na mategemeo yake
Amesema Wanawake wa ndani na nje hawana haja ya kuwa na wasiwasi kwani uwekezaji wa Zanzibar katika Hospital za Serikali ni sawa na Hospital binafsi Bara la Ulaya
Moja ya Watu aliowataja Lusi katika safari yake ya kupata huduma bora ni Muuguzi Maryam na hapa anatueleza hatua hiyo ilivyompa uzoefu na kuongeza maarifa kwa kujisikia fahari katika kazi yake









