KAMATI BLW IMERIDHISHWA NA UJENZI MNADANI DARAJANI

Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi iimeridhishwa na hatua iliyofikiwa ya matengenezo ya Miradi ya Majengo Makongwe inayosimamiwa na Shirika la Nyumba la Zanzibar katika maeneo ya Darajani.

Kamati hiyo ambayo imepokea Taarifa ya Miradi ya matengenezo wa Majengo hayo na kufanya ziara ya kuangalia hatua iliyofikwa, Makamo Mwenyekiti wa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi  Mhe. Aza Januari Joseph amesema inatoa matumaini kwa hatua iliyofikiwa ili kutoa fursa ya kutumika kwa Majengo hayo ya Biashara.

JITIHADA ZA PAMOJA ZINAHITAJIKA KUKUZA SEKTA YA UTALII

Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale na Wadau wa Sekta hiyo wanahitaji kuwa na ushirikiano wa karibu ili kuondosha vikwazo vinavyoikabili Sekta hiyo ikizingatiwa kuwa ni tegemeo kwa Uchumi wa Zanzibar unaochangia zaidi ya asilimia 30 ya pato lake.

Ukatika Kikao kilichohusisha Wizara ya Utalii na mambo ya kale, wakuu wa Mikoa, Wilaya na Masheha, Waziri wa Wizara hiyo mhe. Mudrik Ramadhan Soraga amesema Sekta ya Utalii inakabiliwa na matatizo kadhaa ambayo kutatuliwa kwake kunahitaji nguvu za Wadau mbalimbali huku Serikali ikiwa inafanya mageuzi ikiwemo Sera ili kufikia malengo.

MADEREVA WAMESISITIZWA KUZINGATIA SHERIA

Mamlaka zinazosimamia Usalama wa Barabarani pamoja na Waendesha Pikipiki (bodaboda) wametakiwa kuchukuwa hatua za Kisheria pamoja na kusimamia vyema Ajali zinazojitokeza kila siku.

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Dkt. Khalid Salum Mohamed ameeleza hayo wakati akizungumza na Vyombo vya usalama pamoja na Wawakilishi wa waendesha BodaBoda na kusema kuwa kutokana na ongezeko la Ajali, ni vyema kuzingatia matumizi ya Barabara pamoja na kutii Sheria.

SHIGELA AONGOZA DUA YA KUMUOMBEA HAYATI MZEE MWINYI

    Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela Amewaongoza Mamia ya Waumini wa Dini ya Kiislamu katika Viwanja vya Msikiti Mkuu wa Ijumaa katika Dua Maalumu ya kumuombea Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Hayati Ali Hasani Mwinyi 
    Akiongoza Dua hiyo Maalumu Mkuu huyo wa Mkoa amesema Hayati Mwinyi anakumbukwa kwa mengi lakini kubwa ni kwa kuwaunganisha Watanzania pamoja na kuleta Umoja wa Kitaifa.

DAWA ZA KULEVYA AINA MBALIMBALI KUKAMATA ZANZIBAR.

Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevya Zanzibar, imefanikiwa kukamata Dawa za kulevya aina mbalimbali zinazokadiriwa kufikia Kilo  Mia Moja na Ishirini na tano.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Kanal Burhani Zuberi Nassoro, amesema Dawa hizo zimekamatwa katika Operesheni  iliyofanyika Mwezi January katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mjini Magharibi.

WAZAZI NA WALEZI KUENDELEZA MASHIRIKANO YA PAMOJA NA WALIMU.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab

Amewataka Wazazi na Walezi Kisiwa Pemba kuendeleza  mashirikano ya pamoja na Walimu katika kuwasimamia Watoto wao  kusoma ili   Taifa lipate  Watalamu wa Fani mbali mbali.

Ametowa Wito huo huko Skuli ya Dkt Salamu Ahmed Ndugu Kitu Chake Chake katika Mahafali ya Wanafunzi wa Kidatu cha Nne.

DKT SAMIA AMEWASILI NCHINI JAKARTA KWA ZIARA YA KIKAZI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Soekarno-Hatta, Tangerang Mjini Jarkata Nchini kwa ajili ya ziara ya Kitaifa Nchini Indonesia inayoanza 24 Januari, 2024.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Soekarno -hatta, Tangerang Raisi Samia alipokelewa na Naibu Waziri wa mambo ya Nje wa Indonesia Vice Pahala Nugraha Mansury.

Ziara hio ya siku tatu imekuja kufuatia mualiko wa Raisi wa Indonesia Mh. Joko Widodo ambae alifanya ziara Nchini Tanzania Agosti 2023.

 

MKAKATI WA SERIKALI KUSISITIZA UTALII WA KIMAZINGIRA IMELENGA KUHAMASISHA WATALII WA DARAJA LA JUU KUINGIA NCHINI KWA IDADI

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mh Simai Mohamed Said, amesema Mkakati wa Serikali kusisitiza Utalii wa kimazingira imelenga kuhamasisha Watalii wa Daraja la juu kuingia Nchini kwa idadi Nchini.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa eneo la Ujenzi wa Hoteli ya Four Seasons katika Kijiji cha Pongwe Pwani, amesema kuna Watalii wenye uwezo mkubwa wanahitaji kukaa katika Hoteli zenye mazingira ya asili. 

AMEAGIZA KUPEWA KIPAUMBELE WAFANYABIASHARA WALIOKUWEPO AWALI WAKATI SOKO LA MWANAKWEREKWE LITAKAPOKAMILIKA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Mwinyi meyasema hayo katika muendelezo wa shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Mwinyi ameweka jiwe la msingi ujenzi wa Soko la kisasa Mwanakwerekewe ambapo amezitaka mamlaka husika kuhakikisha kuwa licha ya maombi mapya ya wafanyabiashara katika soko hilo, wahakikishe wafanyabiashara waliopisha ujenzi wanazingatiwa.

 

WAWEKEZAJI WAZAWA KUANZISHA MIRADI MIKUBWA YA HOTELI ZA NYOTA TANO.

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira Dkt Suleiman Said Jafo amesema mabadiliko makubwa yanayofanywa na Serikali katika ujenzi wa miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege ni sehemu ya kukuza sekta ya uwekezaji.

Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi Hoteli ya Kiwengwa Tembo Beach Hotel and  Resort, ikiwa ni shamra shamra za miaka 60 ya mapinduzi amesema hatua hiyo inafikia dhamira sahihi ya kufanyika Mapinduzi ili kuleta mabadiliko ya kiuchumi.

 

Subscribe to News
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.