TANESCO LINDI YAONGEZA UWEZO WA KITUO CHA MAHUMBIKA KUKIDHI MAHITAJI YA UMEME
Kutokana na ongezeko la mahitaji ya Umeme katika Mikoa ya Lindi na Mtwara, Shirika la Umeme tanzania (TANESCO) Mkoa wa Lindi limeanzisha mradi wa kuongeza uwezo wa kituo cha kupooza umeme cha maumbika kwa kufunga transfoma yenye uwezo wa zaidi ya megawati 15 kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 702.
