WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA KUSUKUMA NA KUHIFADHI MAJI MWANZA

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, ameweka jiwe la msingi la Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Kusukuma na Kuhifadhi Maji katika mkoa wa Mwanza, mradi unaolenga kuboresha usambazaji wa maji safi na salama kwa wananchi.

WATENDAJI KITUO CHA UOKOZI MWANZA WATAKIWA KUTOA HUDUMA ZA DHARURA KWA SAA 24

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, ametoa maagizo kwa watendaji wa Kituo cha Kuratibu. Utafutaji na Uokozi cha Kikanda – Mwanza, chenye thamani ya takribani shilingi bilioni 19.8, kuhakikisha kituo hicho kinaendeshwa kwa saa 24 na kwa ufanisi wa hali ya juu.

Amesema hayo leo Januari 23, 2026 baada ya kutembelea kituo cha Kuratibu Utafutaji na Uokozi, jijini Mwanza. Huku akisisitiza kuwa huduma za uokozi ni kazi ya kuokoa maisha, hivyo hakuna uvumilivu kwa uzembe, kuchelewesha utoaji wa huduma za msaada pindi inapohitajika.

Subscribe to Mwanza Tanzania
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.