ZANZIBAR INAENDELEA KUPIGA HATUA KWENYE SEKTA YA UTALII KIMATAIFA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, Dkt. Aboud Suleiman Jumbe Akizungumza katika tathmini ya utekelezaji wa siku 100, amesema Zanzibar imeendelea kufanya vizuri na kujipatia nafasi kwenye orodha mbalimbali za kimataifa za utalii.
Ameeleza kuwa Zanzibar sasa ipo katika kumi bora barani Afrika kwenye vivutio vya utalii, miradi bora ya kitalii, maeneo bora ya honeymoon pamoja na michezo ya baharini, hali inayoongeza ushindani na kuimarisha nafasi ya Zanzibar katika soko la kimataifa la utalii.



