BULGARIA AIR YAANZA RASMI SAFARI ZAKE ZANZIBAR

Mapokezi ya Shirika la Ndege la Bulgaria Air (Bul Air) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume (AAKIA)  Alhamis ya Tarehe 22 Januari 2026

Ndege Aina ya Airbus a 320 iliwasili Uwanjani hapo Majira ya saa 5:30 Asubuhi ikitokea Jijini Sofia ikiwa na Jumla ya Abiria 180.

Shirika hilo la Ndege sasa limeanza rasmi safari zake na linatarajiwa kuwasili Zanzibar MaraTatu kwa Mwezi.

ZANZIBAR YAJITANGAZA KIUTALII LONDON

 Kwa mara ya kwanza katika historia ya Zanzibar imezindua Matangazo ya Utalii katika Jiji la London Nchini Uingereza kwa kubandika Matangazo yanayosomeka Tembelea Zanzibar kwenye Mabasi maarufu ya Abiria yanayoitwa London Buses.    Hatimaye historia imeandikwa.

 Mabango makubwa yanayochagiza, kushajihisha na kuuvutia Utalii wa Zanzibar yameanza kuonekana Leo kwenye Mabasi ya Abira maarufu kama London Luses Nchini Uingereza.

Subscribe to Kamisheni ya Utalii Zanzibar
 

Simplenews subscription

The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.