POLISI TANZANIA KUSHIRIKIANA NA POLISI WA NCHI ZA FALME ZA KIARABU

KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad amesema Ushirikiano wa Kidiplomasia kati ya Tanzania na Nchi za Falme za Kiarabu kutatoa fursa za kubadilishana uzoefu baina ya pande mbili hizo na  kuimarika kwa ulinzi katika Miradi ya maendeleo Nchini. 

Akizungumza na Balozi mdogo wa Nchi za Falme za Kiarabu  Mhe. Saleh Ahmed Alhemeiri, CP Hamad ameomba uwezekano wa kuongezewa taaluma kwa Askari wa Jeshi la Polisi  kuhusiana na makosa ya Kimtandao makossa ambayo yamekuwa changamoto Duniani.

Balozi mdogo wa Nchi za Falme za Kiarabu Mhe. Saleh Ahmed Alhemeiri amesema ziara yake makao Makuu ya Polisi Zanzibar ni kuendeleza ushirikiano wa Kihistoria baina ya Tanzania na Nchi za Falme za Kiarabu na ameahidi kuimarisha ushirikiano wa Majeshi ya Polisi baina ya Tanzania na UAE.

stories
standard
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.