Habari

MWENGE WA UHURU KUTEMBELEA ZAIDI YA MIRADI 23 KATIKA MKOA WA MJINI MAGHARIBI

     Jumla ya miradi 23 ya zaidi ya Billion 5 inatarajiwa kutembelewa na Mwenge wa Kitaifa wa Uhuru 2024 kwa Mkoa wa Mjini Magharibi.

    Akizungumza katika mapokezi ya Mwenge huo huko Uwanja wa Ndege Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Idrissa Kitwana Mustafa amesema mbio za Mwenge wa uhuru, Mkoani humo zitahusisha kilomita 104 na kutembelea miradi 23 ya maendeleo.

SUZA YATILIANA SAINI HATI YA MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO NA CHUO CHA TAIFA CHA UTALII (NCT)

      Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kimetiliana Saini hati ya makubaliano ya ushirikiano na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) wakilenga uimarishaji wa Sekta ya Elimu katika masuala ya Utalii na kukuza Sekta hiyo.

NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI YA ANGA

     Mkurugenzi Mkuu wa Anga Kenya Emile Ngunza Arao amesema mazingira raifiki yaliyowekwa katika Sekta hiyo Nchini humo, yamekusudia kuwawezesha Wwananchi kutumia Usafiri wa Anga.

     Akizungumza na Vyombo vya Habari baada ya kufunga Kongamano la Sita la Usafiri wa Anga la Jumuiya ya Afrika Mashariki, amesema moja ya uimarishaji huo ni kupunguza Bei ya Tiketi ili kuwezesha Wananchi wa Vipato vyote kumudu gharama za usafiri wa Anga.

WANAFUNZI WA ZANZIBAR KUPATIWA FURSA ZA MASOMO NCHINI POLAND

      Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh.Lela Mohammed Mussa amesema Wizara hiyo itahakikisha inawatafutia Wanafunzi wenye fursa za kusoma Nchi mbalimbali ili kuona wanapata taaluma zitakazowasaidia katka kuleta maendelo ya Nchi. 

    Akizungumza na Waandishi wa Habari Mh.Lela amesema amepokea ujio wa Balozi wa Poland aliyekuja kwa lengo la mahusiano katika Sekta ya Elimu ya juu kwa Poland na Zanzibar ili Wanafunzi wa Zanzibar wapate ufadhili wa kusoma fani tofauti ambazo zinaenda na sayansi na teknolojia. 

VYAMA VYA SIASA VIMEOMBA KUTEKELEZWA KWA VITENDO WANAYOKUBALIANA

    Viongozi wa Vyama vya Siasa wameomba kutekelezwa kwa vitendo falsafa ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kukuza Demokrasia Nchini kwa kuhakikisha hakuna mkwamo wa Kisaiasa kwa maslahi ya Wananchi.

    Viongozi wa Vyama vya Siasa, Asasi za Kiraia na Viongozi wa Dini wanaokutana Zanzibar kwa Siku Mbili katika Kongamano la Demokrasia, wamesema iwapo falsafa hiyo inayohusisha mambo Manne yatafanyiwa kazi yakiwemo ya maridhiano, ustahamilivu na mageuzi ya Demokrasia, itawezesha kufikiwa maridhiano ya Kisiasa Tanzania na kukuza ustawi wa maendeleo.

WAZAZI NA WALEZI MKOANI LINDI WATAKIWA KUTUMIA MIFUMO RASMI KATIKA KUMALIZA MIGOGORO YAO

   Wazazi na walezi Mkoani Lindi wametakiwa kuitumia vyema mifumo iliyowekwa na Serikali katika kushughulikia migogoro na tofauti zinazojitokeza katika familia zao  ambayo kwa kiasi kikubwa uchangia kuachana na  kusababisha watoto kuathiriwa kwa kukosa  malezi imara.

    Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo  katika maadhimisho ya siku ya Familia ambayo kwa ngazi ya Mkoa yamefanyika katika viwanja vya soko la majengo halmashauri ya Mtama Mkoani humo.

WALIMU WATAKIWA KUFUATA MAADILI YA KAZI YAO

     Mkaguzi kata ya Lwenzera Wilaya ya Geita Mkoani Geita amewataka Walimu Wa Shule ya Sekondari Bugando Kufuata Maadili ya Kazi huku akiwataka kutambua kuwa Jamii inawategemea katika kuwafundisha na kutoa malezi Mema kwa Wanafunzi.

     Hayo yamebainishwa na Mkaguzi wa Kata hiyo Mkaguzi Msaidizi wa Polisi A/INSP, Pili Kulele wakati alipotembelea Shule hiyo ambapo amewaomba walimu kujikita katika kuwafundisha wanafunzi na kutoa malezi mema ili wawe msaada katika Jamii na kata hiyo kwa ujumla.

WAZIRI WA BIASHARA AAHIDI KUTOA MASHIRIKIANO KWA BARAZA LA UDHIBITI MFUMO WA UTOAJI LESENI

    Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Mhe.Omar Said Shaaban ameahidi kutoa ushirikiano kwa Baraza la Udhibiti Mfumo wa Utowaji wa Leseni ili kufikia malengo ya kuweka mazingira mazuri ya kibiashara nchini.

    Ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Bodi Mpya ya Baraza la Udhibiti Mfumo wa Utowaji wa Leseni katika ukumbi wa Ofisi za Baraza huku Malindi, Wilaya ya Mjini.

SIKU SABA SERIKALI KUTOA MAAMUZI UWEPO WA SOKO LA MAADINI YA VITO TUNDURU

     Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Ahmed Abbas Ahmed amesema ndani ya siku saba kuanzia Mei 15,2024,serikali itatoa maamuzi ya uwepo wa soko moja au masoko matatu ya madini ya vito wilayani Tunduru.

    Akizungumza na wanahabari ofisini kwake mjini Songea,Kanali Abbas amesema akiwa katika ziara ya kikazi wilayani Tunduru hivi karibuni aliweza kutembelea masoko ya madini ya  vito ambayo ni soko la Generation,TUDECU na kukagua ujenzi wa soko jipya la madini.

SERIKALI IMEPIGA HATUA SEKTA YA ANGA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Ali Mwinyi, amewataka Wadau wa Sekta ya Anga kuimarisha Mashirikiano ili kuhakikisha Sekta hiyo inazidi kuimarika.

Akifungua Kongamano la Sita la Usafiri wa Anga la Jumuiya ya Afrika Mashariki  katika Hoteli ya Verde Mtoni,Dk.mwinyi, amesema Nchi inajivunia mafanikio yaliofikiwa katika sekta hiyo.

Subscribe to Habari
 
The subscriber's email address.
Stay informed - subscribe to our newsletter.