MWENGE WA UHURU KUTEMBELEA ZAIDI YA MIRADI 23 KATIKA MKOA WA MJINI MAGHARIBI
Jumla ya miradi 23 ya zaidi ya Billion 5 inatarajiwa kutembelewa na Mwenge wa Kitaifa wa Uhuru 2024 kwa Mkoa wa Mjini Magharibi.
Akizungumza katika mapokezi ya Mwenge huo huko Uwanja wa Ndege Zanzibar Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib Idrissa Kitwana Mustafa amesema mbio za Mwenge wa uhuru, Mkoani humo zitahusisha kilomita 104 na kutembelea miradi 23 ya maendeleo.